Friday 1 May 2015
Better Living Aid yatoa wito kwa wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi!
Posted by
Mkala26,
on
01:48
Watangazaji Hamisa Mussa Lubilo na Deogratius Yagomba wa VOT fm 89.0 wakimuuliza maswali mratibu wa asasi ya Better Living Aid walipomualika leo asubuhi katika kipindi cha Meza huru! |
Mkala Fundikira akijibu moja ya maswali yaliyoulizwa na watangazaji wa kipindi cha Meza huru, kipindi kinachoruka ktk kituo cha redio cha VOT fm 89.0 ya Tabora leo asubuhi. |
Mkala akiwa amevalia fulana yenye ujumbe wenye kupinga mauaji kwa watu wenye ualbino ya mkakati wa Imetosha. |
Fundikira pia alimshukuru Mh Munde Tambwe Abdallah kwa kutoa ahadi ya Mifuko 50 ya simenti, lori 10 za mchanga pamoja na tano za mawe na kokoto , alisema "Tena kabla sijasahau nimpongeze na kumshukuru sasa sana sana Mh Munde Tambwe kwa kutupa msaada ambao ni msingi, kwa maana ya kuwa ahadi yake ndiyo itaanzisha ujenzi wa majengo hayo ya vyoo na zahanati, hivyo basi na wengine wajitolee ili tusonge mbele"
Hoteli ambamo chakula cha usiku cha uchangishaji fedha kwa ujenzi wa vyoo na zahanati utafanyika baadae mwezi huu jijini Dar es Salaam iliyopo maeneo ya Ocean road. |
Aidha asasi hiyo ina mpango wa kuandaa chakula cha usiku jijini Dar es Salaam katika hoteli ya Southern Sun baadae mwezi huu ambapo Mh Samuel Sitta(waziri wa uchukuzi) amekubali kuwa mgeni rasmi, karamu hiyo itaandaliwa ili kuchangisha fedha za kuwezesha miradi hiyo iweze kukamilika. "Bado tupo kwenye hatua za mwanzo za maandalizi lakini tunataraji karamu hiyo ya uchangishaji pesa ifanyike ama mwishoni mwa mwezi wa MEI au mwanzoni mwa mwezi Juni 2015. Pia Fundikira aliwashukuru Mh Aden Ragen(Mbunge wa Tabora mjini), Mh Munde Tambwe(Viti maalum), Sylvester Koka(Mbunge wa Kibaha) na wanachama na wote wa Better Living Aid kwa kuwezesha kifedha upulizwaji wa dawa kijiji cha Amani uliogharimu Tsh Laki 980.
Tembelea mtandao wa betterlivingaid.Blogspot.Com ujue zaidi kuhusu asasi hii na malengo yake au piga namba 0754 666620 kwa maelezo.
Monday 27 April 2015
Better Living Aid co ordinator with friends hand over 100kg of clothes to Amani residents!
Posted by
Mkala26,
on
10:00
Before handing over the aid donated by friends and Millenium village project who donated 100 mosquito nets.
It was 19 August 2013 when me, some Facebook friends and some staff from Millenium Village Projects handed over to Amani village chairman Mr George Lusambilo some 100 kg of used clothes, sweat shirts, 25 kg of maize flour, soap bars and 100 mosquito nets from Millenium Village Projects. It took me some 3 months to collect clothes from friends after I started a group in Facebook called Clothing for elderly with leprosy now known as (Better Living Aid) specially for that reason.
|
This pack of used sweat shirt was donated by a Samaritan, contained more than 100 sweat shirts. |
Here I was counting some donated pairs of shoes |
More donated used clothes |
After hand over of clothes, mosquito nets and food we took a picture with some Amani residents |
Sunday 26 April 2015
Blog's mission
Posted by
Mkala26,
on
04:23
We started this English written blog to facilitate foreign donors with what we do and what we plan to do in the future
My name is Mkala Fundikira (43) I was touched by hardship the Amani villagers are facing. So I decided to collaborate with friends from social sites like Viber and Facebook so that together we can help to improve their lives through different ways including, funding from various foundations, big companies and our own donations
How I found out about Amani village
In year 2013 I happen to arrange Redds Miss Tabora 2013, beauty pageant. In that year Miss Tabora committee decided to involve contestants with social work like visiting orphanges and helping elderly people with basic needs. After the pageant the committee took all contestants to Amani village to visit the elderly and comfort them and provide them with soap bars, sugar and maize flour. That's when my eyes were opened to see these old people living in hardship like not having enough clothes and filthy toilets
The winners of Redds Miss Tabora 2013
Because the pageant show was performed by Ommy Dimpoz one of the most famous musician in the country, we took advantage to take him with us, he was really moved by the conditions at the vllage and promised to do something about toilets at the village.
|
Asasi ya Better Living AID yagharamia upulizwaji wa dawa ya kunguni kijijini Amani!
Posted by
Mkala26,
on
02:50
Kijji cha Amani kinavyoonekana |
Naye afisa ustawi wa jamii mkoa Bw Charles Makoye alisema "kwa niaba ya serikali naishukuru sana tasisi hii ya Better Living Aid kwa jitihada zao za kuboresha maisha ya wakazi wa hapa kijijni na napenda kuchukua nafasi hii kutoa wito kwa makampuni na taasisi nyingine kusaidia kijiji hiki kwani ustawi wa jamii si suala la serikali peke yake bali ni la jamii nzima inayotuzunguka kwani hawa wazee wametoka huko huko katika jamii zetu.
Mratibu wa taasisi ya Better Living Aid ametoa wito kwa makampuni na watu binafsi kuiunga mkono taasisi hiyo katika jitihada zake za kuwajengea vyoo na zahanati wakazi wa kijiji hicho. Vile vile ameeleza dhamira ya taasisi hiyo kutafuta wafadhili ili kujenga zahanati katika kijiji cha Masweya, wilayani Ikungi mkoa wa Singida alisema "Nilipata kufika kijijini Masweya mapema mwaka huu ambako nilipata kujua kwamba wakazi wa hapo hulazimika kutembea km 30 na ushee kwenda kjiji cha Mtunduru kupata huduma za matibabu. Hivyo Better Living Aid itafanya kila liwezekanalo kijiji hicho kipate zahanati japo mdogo ya kuweza kuhudumia wagonjwa wa Malaria nk pia zahanati iweze kutoa huduma kwa wazazi, kitu mambacho kwa sasa hakipo kjijini Masweya.
Shukurani za dhati ziwaendee Mh Munde Tambwe (viti maalum Tabora), Mh Aden Rageh (Mbunge Tabora mjini) Bibi Joha Masawe, Bi Mtagwa Fundikira, Bibi Jamila Kaimika, Bibi Celina Koka na wanachama wote wa kundi la Better Living Aid Tunashukuru kwa msaada wa hali na mali iliyowezesha kijiji cha Amani kufanyiwa fumigation bila kumsahau mtaalamu Bw Selemani Muhogo wa kampuni ya SILVER ENTERTRADE LIMITED aliyepulizia dawa hiyo.
Baadhi ya magodoro ya wakazi hao yakiwa yametayarishwa kwa kupuliziwa dawa |
Bw Muhogo akiandaa mashine ya kupulizia dawa |
Hpa akianza kunyunyiza dawa kwenye magodoro |
Job DONE |
Baadhi ya vyoo vya hapo kijijini |
Mzee Hamisi Husseni akisubiri vifaa vyake vitiwe dawa |
Badhi ya mizigo ya wakazi wa kijiji hicho |
Afisa ustawi wa jamii Bw Charles Makoye akiongea na mkazi wa kijini hapo. |
Bibi Theresia Joseph akiwa nje ya chumba chake akisubiri huduma ya kupuliziwa dawa ya kuuwa kunguni na wadudu wengine. |
Rundo la mahindi likiwa limotolewa nje kupisha upulizaji dawa ya kuua kunguni nani ya chumba yalimokuwa yamehifadhiwa. |
Baadhi ya panya waliokutwa ndani ya chumba cha mkazi mmoja wa kjijini hapo leo. |
Blogger wa Aloyson.com akiwa na Mzee Hamisi Husseni |
Mratibu wa taasisi ya Better Living Aid Mkala Fundikira kushoto akiwa na mwenyekiti wa kijiji cha Amani Bw George Lusambilo baada ya zoezi la upulizaji dawa ya kuuwa wadudu kunguni waliokuwa wakwasumbua mno wakazi wa kijiji hicho cha wazee wasiojiweza na waathieika wa ugonjwa wa ukoma. |
Baada ya ya kupuliziwa dawa baadhi ya kunguni wanaonekana wakiwa wamekufa. |
Blogger Juma Kapipi wa JHabari blog akiongea na mhanga wa kunguni baada ya kumhoji |
Baadhi ya nguo zikichomwa moto baada ya kukutwa na kunguni wengi kupita kiasi. |
Subscribe to:
Posts
(
Atom
)